Kati
ya waliokumbwa na adhabu hiyo ni pamoja na walinzi wake wa karibu ambao
wanadaiwa kutojishughulisha kwa lolote wakati kiongozi huyo alipoteleza
na baadaye kuanguka chini.
Likiwanukuu maofisa wa serikali, gazeti la The Standard lilisema
kuwa walinzi hao wamewajibishwa kwa kushindwa kuchukua hatua za dharura
kushughulikia tukio hilo lililosambaa katika mitandao ya kijamii.
Rais
Mugabe ambaye alikutwa na mkasa huo muda mfupi baada ya kuzungumza na
wafuasi wake waliokuja kumpongeza baada ya kuchaguliwa kuwa mwenyekiti
wa Umoja wa Afrika wiki ijayo atasherehekea siku yake ya kuzaliwa
akitimiza miaka 91.
Vyanzo vya habari vinasema kuwa,
Ikulu haikufurahishwa na namna walinzi wake walivyoshindwa kuchukua
hatua za haraka kudhibiti kuenea kwa taarifa za kuanguka kwake.
Taarifa
zimesema kuwa kwa ujumla walinzi wa rais walibweteka kwani kanuni
zinawataka kusimama angalau hatua chache kutoka kiongozi alipo.
“Hili
suala ni kubwa tena lilipaswa kushughulikiwa kwa umakini mkubwa na
hawa walinzi walizembea kwani kanuni namba tatu inayohusu ulinzi kwa
rais inaeleza ni umbali gani wanapaswa kusimama. Ninachoweza kusema ni
kwamba kuna idara nyingi zinaendelea kuchunguzwa, kuanzia Shirika la
Ndege la Zimbabwe lenyewe hadi timu nzima ya walinzi wake.
Sina
uhakika katika hawa waliosimamishwa kama kuna mmoja wao atarejea
kazini,” kilisema chanzo kimoja cha habari kikikariri taarifa kutoka
mtandao wa www.bulawayo24.com. Hata hivyo mtandao huo baadaye ulisema
kuwa taarifa ofisi ya Ikulu imekanusha vikali taarifa hizo.
Taarifa
zaidi zinasema kuwa walinzi hao walikabidhiwa barua za kusimamishwa
kazi mwishoni mwa wiki na kwamba kurejea kwao kutategemea uchunguzi
unaoendelea kufanywa.
Taarifa za kuwa walinzi hao
walikuwa wamesimamishwa kazi zilipata nguvu mpya wakati wa ziara ya Rais
Edgar Lungu wa Zambia aliyekuwa nchini Zimbabwe na kukutana na mwenyeji
wake Rais Mugabe.
Wale waliokuwepo Ikulu walisema kuwa
walishuhudia sura mpya za walinzi wakiwa kando ya Rais Mugabe. Hata
wakati Rais Lungu akiondoka Ikulu, Rais Mugabe hakuambatana naye
kumsindikiza uwanja wa ndege badala yake alisimama mita chache na baada
ya mgeni wake kuondoka alirejea tena ofisini.
Msemaji wa Ikulu George Charamba hata hivyo alipuuza taarifa hizo akisema kuwa ni uzushi unaoenezwa na watu wasiokuwa na tija.
Alisisitiza kuwa hakuna mlinzi yoyote wa rais wala ofisa wa Ikulu aliyesimamishwa kazi kutokana na tukio la kuanguka kwa Rais.
Rais
Mugabe ambaye anatajwa kuwa ni miongoni mwa viongozi wachache barani
Afrika waliokaa madarakani kwa muda mrefu wiki iliyopita alichaguliwa
kuwa mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU) wadhifa ambao ulizua hali ya
wasiwasi kuhusu nafasi ya umoja huo katika jumuiya ya kimataifa.
Hata
hivyo hivi karibuni Umoja wa Ulaya ulisema kuwa utalegeza vikwazo kwa
kiongozi huyo ili aweze kuhudhuria baadhi ya mikutano ya kikanda hasa
ile inayohusu Umoja wa Afrika na jumuiya ya kimataifa.
No comments:
Post a Comment