Showing posts with label politics. Show all posts
Showing posts with label politics. Show all posts

Irregularities mar CCM preferential polls in Nkasi


EIGHT CCM cadres who are seeking nomination for parliamentary seat in Nkasi North constituency, Rukwa Region have called upon the postponement of preferential polls for the Mkinga Ward due to numerous irregularities including acts of corruption they discovered during rounds of intraparty meetings in the area.

They maintained that if the polls are not postponed they would not concede the results.

The eight aspirants jointly filed a report expressing their grievances and signed it and subsequently handed it officially to the Nkasi CCM District Secretary, Mr Seleman Mahmoud in Namanyere town.

When contacted for comments, Mr Mahmoud admitted to have received it, and that he would hand it over to the CCM district officials for further action.

He acknowledged that he had held preliminary meetings, cautioning them to strictly observe the set norms and regulations during rounds of intraparty meetings they were planning to conduct.

The eight aspirants who signed the complaint include Hypolitus Matete, Rukwa CCM Region Chairperson, Ponsiano Nyami, the Babati DC, Ephraim Kalimalwendo, retired District Executive Council Director Salvatory Seko, the outgoing Nkasi deputy District Council Chairperson.

Others are January Kilamtinde, civil servant, Basil Mbwilo, the outgoing Kipili Ward Councillor, Jastus Shauri and Raphael Siumbu, a civil servant.

The incumbent MP for the Nkasi North constituency Ally Keissy did not attend the meeting even when he was invited.

According to the written grievance report whose copy was availed to the ‘Sunday News’, the nine aspirants accused Mr Kessy of possessing a large amount of cash during the intraparty meetings.

Kubenea heads for Chadema nomination in Ubungo


Chadema’s Ubungo parliamentary aspirants (from
Chadema’s Ubungo parliamentary aspirants (from left) Saed Kubenea, Godluck Mollel and Paul Luhada wait before primary polls take place yesterday at Kimara in Dar es Salaam.PHOTO |SALIM SHAO 
 
 
Dar es Salaam.

 Hali Halisi managing editor Saed Kubenea is headed for nomination as the Chadema parliamentary candidate in Ubungo after emerging victorious in primary polls yesterday.

In the party’s primaries held at Api Forest at Kimara Baruti, Mr Kubenea obtained 61 votes (71 per cent) against his competitors Goodluck Mollel who got 20 votes and Paul Luhada who got four votes out of 85 votes cast.

Speaking to this paper, Mr Kubenea expressed his gratitude to the voters and promised to ensure the constituency remains under Chadema.

Ubungo’s outgoing MP John Mnyika is now running for the newly established Kibamba seat.
“I want to assure my fellow party members that I will not allow this constituency to go to any other party,” he said.

But primaries were postponed in Kibamba where Chadema voters were set to vote for their aspirants, including Mrt Mnyika, yesterday.

One of the candidates who did not want his name mentioned said he was surprised that the polls were postponed and no reason was given for that. He suspected that the move aimed at favouring some aspirants.
“We prepared for the election today but when we arrived here we were told it had been shelved because some of the aspirants were not informed… there are must be something,” he said.
Six Chadema members have picked up forms seeking party nomination for Kibamba.

Former Arusha Mayor leaves ruling party for Chadema

The former mayor for Arusha Municipality, Mr Paul Lotta Laizer, has joined the Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), after defecting from the CCM ruling party.

Mr Laizer, who used to represent Baraa Ward as Councillor, left his former CCM party, and has enlisted with Chadema just as Arusha and other parts of the country are preparing for the forthcoming October 2015 elections.

“I have decided to embrace the winds of change by moving on to another political vessel,” said Laizer upon receiving a membership card from the opposition camp on Friday.

The aspirant was recently relieved of his duties by the Chama Cha Mapinduzi (CCM) after being accused of selling off a piece of land under dubious circumstances.

Paul Lotta Laizer once served as Mayor for Arusha Municipality from 2000 to 2007. Mayor Laizer was relieved off his duties alongside the former Sombetini Ward Councillor, Mr Mussa Mkanga.

Since then Mr Laizer has been trying to make political comeback without much success until now that he decided to leave his former party joining the opposition.

After the deal went sour, the Ms Ermoil Marketing Co. Ltd filed a suit and demanded 245 million shillings in damages through the local commercial court.

Development of the plot number 68, of Block ‘W’ in area ‘F,’ which stands across the Dodoma road from Summit Business Centre and opposite the Kilombero market in Levolosi area, remains at a standstill, eight years later.

CCM nomination polls in Tarime postponed over rigging allegations

CCM nomination polls for parliamentary and councillor posts in Tarime rural and Tarime urban constituencies were on Saturday postponed after many ballot papers were allegedly caught already voted in favour of some candidates.

“The polls have been postponed until today. Many ticked ballot papers have this morning been confiscated.

We want each ballot paper to be ticked by one person not one person ticking hundreds of ballot papers”, Tarime District CCM chairman Mr Rashid Bogomba told angry CCM supporters when announcing the decision at the party’s office here on Saturday.

According to him, over 4,000 ballot papers were found ticked in Tarime rural and over 2,000 found ticked in Tarime urban. He named some stations caught with ticked ballot papers as Nyanungu, Nyamwaga, Sirari, Mbogi, Magena and Nyamongo.

The District CCM chairman appealed for calm among the party members and get ready for voting today (Monday). “We are changing the supervisor of the election and you will be informed today”, he said.

Dozens of police officers were deployed at the district CCM office to prevent any possible violence acts. At the same time the Tarime District CCM Secretary, Mr Barnabas Nyerembe, was picked by officials from the Tarime District Prevention and Combating Corruption Bureau (PCCB) under tidy security for questioning in connection with the incident.

Some CCM members called for immediate removal of the District CCM secretary on ground that he was behind the deal. Efforts by the ‘Sunday News’ to get the District CCM Secretary for comment failed after he was picked from his office by PCCB officials.

Acting Regional Police Commander for Tarime/ Rorya Sweebert Njewike was not available to give detailed information about the matter.

“I am currently on my way to Tarime from Mwanza and I will issue my report after arriving”, the acting RPC said when reached for comment over phone.

Mauzauza kura za maoni CCM
















 Dar es salaam
 Mauzauza jana yalitawala mchakato wa kura za maoni kwa ajili ya kupata wagombea ubunge na udiwani kwa tiketi ya CCM kutokana na kuwapo kwa vitendo vya rushwa, vurugu, kura kuchomwa moto, makada kukamatwa, wanachama kutoruhusiwa kupiga kura na kugundulika kwa karatsi zilizokwishapigwa kura.

Kwenye baadhi ya maeneo kazi hiyo iliahirishwa hadi leo kutokana na vifaa kuchelewa na pia tatizo la kugundulika kwa shahada ambazo zimeshapigwa kura zikiwa ndani ya maboksi.

Lakini matukio yaliyotawala kura za maoni ni makada kukamatwa kwa tuhuma za kujihusisha na vitendo vya rushwa kwa kugawa fedha au kuchapisha karatasi bandia za kupigia kura.

Dar es Salaam

Wilayani Kinondoni jijini Dar es Salaam, Takukuru inawashikilia wagombea sita kwa tuhuma za kutoa rushwa kwa wajumbe ili wachaguliwe kwenye kura za maoni.

Makamu mkuu wa Takukuru wilayani Kinondoni, Denis Manumbu aliwataja waliokamatwa kuwa ni katibu wa kata ya Kibamba, Denisi Kalela, katibu wa itikadi, Babu Kimanyo, diwani wa viti maalumu wa Goba, Rehema Luhanja,
Wengine ni mwenyekiti kata ya Goba, Pili Mustafa, mgombea udiwani, Msigani Mwasha na Eliasi Nawera ambaye anagombea ubunge Jimbo la Kawe.

Alisema kuwa Kalela, na Kimanyo walikamatwa juzi saa 4:00 usiku maeneo ya Kibamba CCM, huku Mustafa na Luhanja wakikamatwa maeneo ya Goba Kati na Kawe.

“Walikamatwa wakiwa wanatoa rushwa na wengine walikamatwa wakiwa na kiasi cha pesa ambazo bado walikuwa wanazigawa huku wengine wakiwashawishi wajumbe kupokea rushwa,” alieleza Manumbu.

Manumbu alisema katika kipindi hiki cha uchaguzi ofisi yao inafanya kazi saa 24 ikipokea taarifa zote zinazohusu rushwa.

Kondoa

Lakini hali ilikuwa mbaya wilayani Kondoa, Dodoma ambako CCM ililazimika kuchoma moto makasha sita ya kupigia kura baada ya kubainika kuwa baadhi ya wanachama walitumia kadi ya CCM pekee bila ya kitambulisho cha kupigia kura.

Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Shaaban Kissu, mwenyekiti wa CCM wa wilaya, Othman Gora na kamanda wa polisi wa wilaya, Nyantora walikubaliana kuchomwa moto baada ya kubaini tatizo hilo.
Hatua hiyo, inatokana na wanachama kuanzisha zogo kuwa vitambulisho vya kura havikutumika kabla ya uamuzi huo kufikiwa. Tayari zaidi ya wanachama 200 walikuwa wamepiga kura hizo.

Maboksi hayo yalichomwa mbele ya kituo cha kupigia kura cha Ubembeni na kushuhudiwa na wananchi, wananchama wa CCM, polisi na uongozi wa CCM.

Baada ya kuyachoma, Kissu alitangaza kuahirishwa kwa uchaguzi huo baada ya dosari hiyo na kwamba utarudiwa leo.

Baadaye kamanda wa polisi wa wilaya aliamrisha watu wote kutawanyika eneo hilo hadi leo.
Awali kulitokea vurugu baada ya baadhi ya wanachama kunyakua sanduku lililokuwa na kura na kutaka kukimbia nalo kwa tuhuma kuwa mawakala hawakuwa wakitenda haki kwa wapiga kura

Mbeya

Kashfa ya matumizi ya rushwa pia ilijitokeza mkoani Mbeya ambako mgombea udiwani mmoja kulalamikiwa kwa madai ya kuwakodisha wanafunzi wampigie kura kwa malipo ya Sh2,000 kwa kila mmoja.

Mgombea huyo wa udiwani wa Kata ya Mbalizi Road analalamikiwa pia alikwenda kwenye kilabu za pombe kuwatafuta watu wanaotaka kumpigia kura ili awanunulie kinywaji.
Miongoni mwa walalamikaji ni Ally Salum na Aziza Mbika wa eneo la Sabasaba ambao walisema walimwona mgombea huyo akitoa fedha na pombe kwa vijana mbalimbali .

Msimamizi wa uchaguzi wa Kituo cha Meta, Ndoni Mwakalukwa alikiri kupokea malalamiko ingawa hakushuhudia utoaji wa fedha hizo na kwamba atayazungumza baada ya kumaliza kazi ya upigaji kura.

Vituo vingine, vikiwamo vya Kata za Ruanda na Sinde, vilikosa wanachama wa kupiga kura na badala yake walifika mmoja mmoja kila baada ya saa kupita.

Wasimamizi wa uchaguzi maeneo hayo walikuwa na kazi ngumu ya kuwaita watu waliokuwa wakipita wakiwaomba wakapige kura kama ni wanachama wa CCM.

“Tatizo ni kwamba vituo vya kupigia kura havijawekewa alama yoyote, hivyo wanachama wengi hawajui,’’ alisema msimamizi wa kituo cha Soweto, Ambakisye Kitunga.

Lindi

Rushwa pia ilijitokeza kwenye Jimbo la Mchinga (CCM) ambako mbunge wa viti maalumu, Fatuma Mikidadi alikamatwa na Takukuru kwa tuhuma za kutoa rushwa kwa wafanyakazi wa taasisi hiyo waliomkamata kwa tuhuma za hongo.

Habari zinasema kuwa mgombea huyo alikutwa na wafanyakazi wa Takukuru akitoa rushwa kwa wanachama wa Kata ya Mchinga.

Alipotakiwa kuzungumzia tuhuma hizo, Mikidadi alikasirika akisema: “Uongo, uongo, huu ni uzushi kabisa.”

Alipoulizwa kwa nini anafikiri wamemsingizia, alisema: “sijui hawa wanasingizia singizia tu, uongo.” Hata hivyo, kamanda wa Takukuru wa mkoa wa Lindi, Steven Chami alisema Fatuma alikamatwa saa 5:00 usiku Kata ya Mchinga akigawa fedha kwa wanachama.

Chami alisema akiwa ofisi za Takukuru baada ya mahojiano, mtuhumiwa huyo alitoa tena Sh780,000 kwa ajili ya kuwahonga maofisa hao ili wasiendelee na suala hilo.

Alisema kutokana na kitendo hicho, Takukuru itamfikisha mahakamani muda wowote baada ya mwanasheria kutafsiri na kubainisha tuhuma zake.

Wakati huohuo, kamanda huyo alisema mgombea ubunge wa Jimbo la Lindi Mjini, Mohamedi Utali alishikiliwa kwa muda wa saa kadha kwa mahojiano na Takukuru baada ya kukutwa na Sh4milioni saa 8:30 usiku akiwa Kata ya Mbanja.

Chami alisema kukamatwa kwa mgombea huyo kulitokana na ushirikiano baina ya wananchi na taasisi hiyo.

Shinyanga

Mjini Shinyanga, katibu wa Kata ya Mjini Shinyanga, Ramadhani Majani amenusurika kipigo baada ya kukamatwa usiku wa kuamkia jana akiwa ofisini kwake na mmoja wa wagombea udiwani na ubunge katika Jimbo la Shinyanga Mjini.

Mashuhuda wa tukio hilo waliwaeleza waandishi wa habari jana kwamba Majani alikutwa na kadhia hiyo baada ya watu waliotilia shaka nyendo zake kwa kitendo chake cha kuongozana na mmoja wa wagombea nyakati za usiku kuingia ofisini na hivyo kuhisi kuna jambo lisilokuwa la kawaida walilopanga kufanya.

Walisema waliamua kuwapigia simu wagombea wengine waliokwenda ofisi hizo na kumkuta mgombea mmoja (jina limehifadhiwa) akiwa anaongea naye, hata hivyo walishituka ghafla baada ya kuona kundi la wana-CCM wakijongea ofisini hapo.

“Sisi tulipigiwa simu usiku saa 4:45 na baadhi ya watu wanaoishi jirani na ofisi yetu ya kata kwamba wamemuona katibu kata wetu akiwa na mgombea udiwani pamoja na wapambe wake. Walidai inavyoelekea walikuwa wakipanga mikakati mibovu ya kutaka kuiba kura,” alisema Rashidi Abdalah.

“Taarifa hizo zilitushangaza sana. tuliamua kuchukua gari na kwenda katika eneo la ofisi na kweli tulimkuta katibu kata akiwa na mgombea (anamtaja jina) wakiwa nje ya ofisi za CCM wakitaka kuingia ndani, ghafla walipotuona mgombea na wapambe wake walikimbia na katibu kata aliingia ofisini na kuufunga mlango,” alieleza aliongeza.

Abdalah alidai kitendo cha Majani kukimbilia ofisini kilisababisha baadhi ya watu kushikwa na hasira na kutishia kuvunja mlango ili kumtoa nje na kumshushia kipigo, lakini mgombea
mwingine alimsihi ajisalimishe na kufanikiwa kutuliza ghasia.

Majani alikiri kutaka kupigwa na kundi la wana-CCM na kwamba ni kweli muda huo wa usiku alikuwa ofisini akifanya kazi ya kugonga muhuri kwenye karatasi za kupigia kura japo hakuweza kufafanua kitendo cha mmoja wa wagombea kuwa katika maeneo hayo nyakati hizo za usiku.

“Nilikuwa naendelea na kazi zangu lakini baadaye nilishangaa watu wanakuja na fimbo wakidai niko na mgombea ilibidi nijifungie ofisini kwangu,” alisema Majani.

Handeni
 
 Hali ya sintofahamu ilitanda kwenye tawi la Bomani, Kata ya Vibaoni wakati zaidi ya wanachama 60 walipogoma kupigia kura wagombea udiwani kwa maelezo kuwa hawawafahamu kwa kuwa hawakufika eneo hilo kujinadi na badala yake kuamua kupiga kura ya wagombea ubunge.

Wakizungumza jana wakati wa kuwasubiri wagombea, wanachama hao walisema kuwa walikutana kuanzia saa 9:00 alasiri kwa ajili ya kuwasubiri, lakini hawakutokea hadi saa 12:00 jioni, kitu ambacho walidai kuwa ni dharau.

Mwenyekiti wa mtaa wa Bomani, John Mohamed alisema kuwa walikubaliana kukutana na madiwani hao kwa mara ya kwanza, lakini akidi ya wanachama haikutimia ikawabidi kuahirisha
 kikao hicho hadi jana lakini kitu cha ajabu wagombea hao hawakutokea hadi jioni.

Arusha

Sakata la karatasi bandia za kupigia kura pia liliibuka mkoani Arusha, ambako viongozi wawili wa CCM walikamatwa kwa tuhuma hizo. Waliokamatwa ni katibu wa Kata ya Mjini Kati, Ally Meku na mwenyekiti wa Mtaa wa Bondeni, Yakub Shaban.

Katibu wa Wilaya ya Arusha, Feruz Bano alisema: “Ni kweli wamekamatwa, lakini tunafuatilia kujua kosa lao kwa kuwa hawana ofisi, hivyo walikuwa wanapeleka karatasi hizo kwenye chumba cha kupigia kura kidogo kidogo,” alisema.

Dodoma

Rafu iligubika uchaguzi huo mkoani Dodoma ambako baadhi ya wanachama walikamatwa na shahada bandia, huku vurugu zikiripotiwa maeneo kadhaa.

Waliokamatwa na tuhuma kuwa walikuwa na shahada bandia ni katibu wa vijana Tawi la Chang’ombe, Nasra Salum akiwa na shahada 20 za kupigia kura, 20 za udiwani, Bakari Fundikira (za ubunge), na David Malolle.

Mwingine aliyekamatwa kwa tuhuma hizo ni Faisi Mussa ambaye CCM imeeleza alikutwa na shahada 15 bandia.

Aidha, baadhi ya kata zilishindwa kufanya uchaguzi kutokana sababu mbalimbali ikiwemo kuchelewa kwa vifaa na karatasi za kupigia kura kuwa na makosa. Miongoni mwa kata zilizoshindwa kufanya uchaguzi huo ni Tambukareli na Kilimani mjini Dodoma.

Katibu wa CCM wa mkoa, Albert Mgumba alisema kata ambazo hazijafanya uchaguzi, kazi hiyo itafanyika leo kabla ya saa 4:00 asubuhi. Kuhusu makada waliokamatwa, katibu huyo alisema jambo hilo waulizwe makatibu wa wilaya kwa kuwa ndiyo wasimamizi wa uchaguzi huo.

Katika hatua nyingine, vurugu zimetokea katika tawi la Mji Mpya lililoko Kata ya Uhuru kutokana na baadhi ya wanachama kudai kuna mamluki wameingia kupiga kura.

“Asubuhi walikuja watu kutoka Tawi la Uhuru wakidai kuwa kuna mamluki wanataka kupiga kura kwenye tawi letu, lakini baada ya viongozi kufika tulirekebisha na zoezi likaendelea kwa amani na utulivu,” alisema msimamizi wa kituo hicho, Mariam Jumbe.

Bukoba

Hali ilikuwa tofauti mkoa Kagera ambako uchaguzi huo majina ya wanachama waliofariki dunia yalikuwapo kwenye orodha ya wapiga kura Jimbo la Nkenge huku kukiwa na hofu ya kuanguka kwa vigogo.

Hali hiyo ilitokea katika vituo vya Mutemba na Igayaza. Hata hivyo, katibu wa CCM wa Wilaya ya Missenyi, Mwajuma Mboha alisema kujulikana kwa majina hayo, ni matunda ya uwepo wa mawakala katika uchaguzi huo.

Pia kumekuwa na tatizo la kukosekana kwa majina ya baadhi ya watu waliofika kupigakura. Katika kata hiyo ya Nsunga kulikuwa na watu saba waliolalamikia kutoorodheshwa.

Mtwara

Kukosekana kwa majina katika orodha ya wapigakura pia ilijitokeza kwenye Manispaa ya Mtwara Mindindani.

Wakiongea na Mwananchi, Shangani Aisha Ismail na Salima Nassoro wa Tawi la Vigaeni walisema wanashangazwa na kitendo cha uongozi wa CCM kuwapa kadi za chama bila kuweka majina yao katika daftari la wapigakura.

“Sisi tumepewa kadi tunazo mikononi hatujui kama nyingine zimesajiliwa au la. Nyingine tumezilipia na majina yetu hayapo. Kuna kadi nyingine za mwaka 2000 hadi mwaka 1950 zipo na majina yao yapo na sisi majina yetu hayapo kuna nini hapa?” alihoji Aisha
Katibu wa itikadi na uenezi wa wilaya, Mohamed Watanga alikiri kuwapo na tatizo hilo, akieleza kuwa wanalitafutia ufumbuzi.

Njombe

Pia mkoani Njombe, wanachama walishindwa kupigakura kutokana na kadi zao za uanachama kuonekana kuwa zilikatwa baada ya Julai 15, siku ambayo CCM ilifunga kazi ya kuandikisha wanachama wapya.

Msimamizi wa uchaguzi wa kituo cha Mpechi, Sarah Nyandoa alisema licha ya uchaguzi kufanyika kwa amani, alikiri kuwapo kwa wanachama waliokuwa na kazi walizopata baada ya Julai 15.
“Ni kweli kuna baadhi ya watu wanakuja na kadi zao zilizochukuliwa baada ya Julai 18, lakini tumewarudisha baada ya kuwaelimisha wameridhika,” alisema Nyadoa.

Pwani

Mchakato kura za maoni umeingia dosari katika vituo kadhaa baada ya baadhi ya wanachama kukatwa majina yao kwenye daftari la orodha ya wanachama wa chama hicho.

Mbali ya kuwepo majina yaliyokatwa, pia baadhi ya wanachama walikutwa wakipiga kura kwa kutumia stakabadhi ya malipo ya wanachama maarufu badala ya kutumia kadi ya uanachama wa CCM.

Kasoro hizo zilisababisha vurugu kwenye baadhi ya vituo vya kupigia kura mjini Kibaha na kumlazimu mwenyekiti wa CCM Kibaha Mjini, Maulid Bundala kusitisha uchaguzi huo kwenye vituo kadhaa vilivyokua na kasoro.

Bundala alisema jana mchana kuwa vituo vilivyofutiwa kufanya uchaguzi ni Morning Star na Machinjioni vilivyoko Kata ya Tangini mjini Kibaha. Uchaguzi huo utarudiwa leo.
Alipoulizwa sababu za kuwepo tofauti ya idadi ya majina yaliyomo kwenye daftari la uanachama na idadi ya wenye kadi za chama eneo hilo, alisema wamebaini kasoro hiyo imesababishwa na baadhi ya mabalozi kutowasajili kwenye daftari la chama la wapigakura.

Katika hatua nyingine, baadhi ya wanachama waliokuwa wakipiga kura Kibaha Mjini wamelalamikia kuwepo rafu katika mchakato wa upigaji kura wakisema baadhi ya matawi yaliweka orodha kubwa ya wanachama wanaoruhusiwa kupiga kura ikilinganishwa na idadi ya awali iliyobandikwa kwenye kuta za ofisi za matawi yao.

Tarime

Mjini Tarime mkoa wa Mara, uchaguzi ulilazimika kuahirishwa hadi leo baada ya kukamatwa kwa karatasi bandia za kupigia zilizokuwa zimeshawekewa alama ya ndiyo kwa wagombea wa ubunge Jimbo la Tarime, na Tarime Mjini.

habari kutoka ndani ya CCM zinasema kuwa karatasi hizo zinazoendelea kukusanywa, zilitengenezwa na mmoja wa viongozi wa wilaya, Bernard Nyerembe ambaye amekamatwa na kufikishwa Takukuru kwa mahojiano zaidi.

Habari hizo zinasema kuwa karatasi hizo zilikuwa zichanganywe na karatasi halali baada ya wanachama kupiga kura za maoni.

Mwenyekiti wa CCM wa wilaya, Rashid Bogomba alithibitisha kukamatwa kwa karatasi hizo jana asubuhi.

Alisema kwa Jimbo la Tarime, kura hizo zimekamatiwa katika vijiji vya Nyamwaga, Masanga na Nyamongo na kwa Jimbo la Tarime Mjini zimekamatwa Mtaa wa Bomani, Magena na Romori.
Bogomba alisema kutokana na kukamatwa kwa karatasi hizo, uchaguzi umeahirishwa.

Kamanda wa polisi wa Tarime/Rorya, Benadict Mambosasa pia alithibitisha kukamatwa kwa Nyerembe na kwamba amepelekwa Takukuru kuhojiwa. Alisema Nyerembe alikamatwa akiwa ofisi ya CCM ya wilaya baada ya wanachama kumtuhumu kuwa alikuwa na karatasi zilizokwishapigwa kura kwa ajili ya wagombea wawili wa majimbo hayo.

Mwananchi ilipomtafuta Nyambari Nyangwine anayetetea ubunge wa Tarime, na Waziri Gaudensia Kabaka (Tarime Mjini) wote wwalikanusha kuhusika na kudai hizo ni njama zilizopikwa dhidi yao.
Makada wengine wanaowania ubunge wa Tarime ni Christopher Kangoye ambaye ni mkuu wa Wilaya ya Arusha, Nyambari Nyangwine (mbunge), Pius Marwa, John Gimunta, Maseke Muhono, Lucas Mwita, Paul Matongo na Charles Machage.

Kwa jimbo jipya la Tarime Mjini wanaogombea ni Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka, Maico Kembaki, Philipo Nyirabu, Jonathani Machango, Ditu Manko na Brito Burure.
*Imeandikwa na Dinna Maningo, Suzy Butondo, Julieth Ngarabali, Phinias Bashaya, Brandy Nelson, Hawa Mathias, Justa Mussa, Godfrey Kahango, Rajabu Athumani, Mwanja Ibadi, Mussa Juma, Sharon Sauwa, Mary Sanyiwa, Shaban Lupimo, Beatrice Moses na Emma Kalalu.

Food fortification gets underway


THE government has started fortifying foods with folate (folic acid) to reduce incidence of children being born with hydrocephalus, a medical condition of fluid filling in their heads.

Speaking exclusively to 'Sunday News' recently, Muhimbili Orthopaedic Institute (MOI) Executive Director, Dr Othman Kiloloma said that because one cause of hydrocephalus is when women don't eat leafy vegetables when pregnant, fortification is a quick way of addressing nutritional issues.

Hydrocephalus is a brain condition that occurs when cerebral spinal fluid (CSF) -- the clear, water-like fluid that surrounds and cushions the brain and spinal cord -- is unable to drain from the brain.

It then pools, causing a backup of fluid in the skull. Sometimes referred to as 'water on the brain,' hydrocephalus can cause babies' and young children's heads to swell to accommodate the excess fluid.

Older kids, whose skull bones have matured and fused together, experience painful headaches due to increased pressure in the head. "Taking from our experience, the two major causes of this condition is birth related infections and deficiency in folic acids.

The government has been instrumental in fortification and the addition of folate and zinc in the pool of fortified foods is a step in the right direction," he said.

Dr Kiloloma said that it was unfortunate that many women today who get pregnant do not make the required preparations which include choosing the right things to eat. He added that junk foods are causing more problems than what meets the eye.

The Resident Coordinator of the UN System, Mr Alvaro Rodriguez, told this paper that the government and President Jakaya Kikwete had played an instrumental role in striving to address nutritional related challenges and deserved praise.

Mr Rodriguez said that looking at the hydrocephalus problem, being highly specialised that requires specialised solutions like having adequate neurosurgeons and orthopaedics to work together is a long term intervention, the fortification route is a wise one as a short term measure.

According to statistics available from the Association for Spina Bifida and Hydrocephalus Tanzania (ASBAHT), out of every 1,000 births, there are at least two children born with either one or two conditions.

In other words, with the country currently seeing the deliverance of almost one million births annually, this means that almost 2,000 are born with these defects.

The Executive Director revealed that whilst the wait to check the prevalence of the disease since the fortification of folic acid started, they are continuously gathering information and statistics to that regard.

As a way to mark the Nelson Mandela International Day that was organised by the South Africa High Commission in Tanzania and the United Nations Information Centre recently, employees from both offices gathered at the MOI children's ward and provided 67 minutes of community services for children including 25 with big heads.

The Director of Nursing Services, Ms Flora Kimaro, said that incidences of the disease are on the rise and they are seeing this as they receive new cases on a daily basis mostly from upcountry in Iringa, Njombe and Mbinga.

Other regions with high prevalence of these defects include areas where pastoralists are dominant, Mtwara, Lindi, Morogoro, Dodoma and parts of Mkuranga District.

Ms Kimaro said that the increase of cases is such that there are times that the mothers of the children have to share beds but was quick to add that a new children's building is almost complete and that there will be a special ward for these children.

"It is heartening to see these mothers speaking this way and even smiling thanks to this community service. Many of their husbands have left all the responsibility to them and most are totally dependent on whatever food MOI can provide, more people need to lend a hand," Ms Kimaro said solemnly.

The South African High Commissioner to Tanzania, Mr Thami Mseleku, said that the Mandela Day is usually celebrated on July 18 but had to be postponed as it coincided with Eid celebrations.

Mr Mseleku said that the visit to the children's ward would have made Madiba proud because it was in the same fashion that he liked to celebrate in calling on everyone to make Mandela Day an everything in whatever they do.

MOI is the only facility in the country that performs surgeries for spina bifida and hydrocephalus defects and that between 20 and 25 operations are performed on a monthly basis.
A tube like gadget called a shunt is the lifeline of children with hydrocephalus and that they are provided free of charge.

However, because these gadgets are donated to MOI, when they run out, buying from local pharmacies costs 130,000/-, an amount not many can easily afford.

Watu milioni 1.6 wamdhamini Lowassa


 
Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa akipungia wananchi wakati akiondoka kutoka makao makuu ya Chadema Kinondoni, Dar es Salaam jana, baada ya kurudisha fomu ya kugombea urais kupitia chama hicho. Picha na Salim Shao


Dar es Salaam. Kada mpya wa Chadema, Edward Lowassa jana amerejesha fomu ya kuwania urais, huku akifanikiwa kupata wadhamini milioni 1.6, zaidi ya nusu ya kura za urais ambazo chama hicho kilipata kwenye Uchaguzi Mkuu mwaka 2010.

Naibu katibu mkuu wa Chadema Zanzibar, Salum Mwalimu alisema idadi hiyo ya wadhamini inaashiria ushindi wa kishindo, kwa maelezo kuwa inakaribia idadi ya kura alizopigiwa katibu mkuu wa chama hicho, Dk Willibrod Slaa alipogombea urais katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.

Katika Uchaguzi huo, Dk Slaa alishika nafasi ya pili baada ya kupata kura 2,271,941 sawa na asilimia 26.34, huku Rais Jakaya Kikwete akipata kura 5,276,827 sawa na asilimia 61.17.

Lowassa alipochukua fomu za kuomba kuteuliwa kuwania urais kwa tiketi ya CCM, kabla ya kuhamia Chadema, alidhaminiwa na wanachama 870,000 nchi nzima.

Dk Slaa, ambaye hajaonekana hadharani tangu Lowassa ajiunge Chadema, jana hakuwapo kwenye ofisi za chama hicho wakati mbunge huyo wa Monduli alipokuwa akirejesha fomu.

Hakuna kiongozi aliyekuwa tayari kuzungumzia suala lake, lakini baadhi ya maofisa wa Chadema walisema wanaendelea kuchapa kazi.

Kama ilivyokuwa juzi katika hafla fupi wakati Lowassa akichukua fomu, umati mkubwa ulifurika na kusababisha Mtaa wa Ufipa uliopo Wilaya ya Kinondoni kufungwa, watu walijazana tena na safari hii umati huo ukiwa umebeba mabango ya kumsifu Waziri Mkuu huyo wa zamani.

Katika hafla ya jana, makamu mwenyekiti wa Chadema-Bara, Profesa Abdallah Safari alieleza jinsi Chadema ilivyojipanga kuchukua nchi na siyo kushinda ubunge na udiwani pekee na kwamba Lowassa amebakiza hatua mbili tu kuingia Ikulu, jambo walilodai kuwa limeichanganya CCM.

Wakati Lowassa ambaye alitangaza rasmi kujiondoa CCM na kujiunga na Chadema Julai 28 mwaka huu akisubiri kupitishwa na Mkutano Mkuu wa chama hicho utakaofanyika Agosti 4, habari za ndani zinaeleza kuwa vigogo kadhaa wa CCM watatambulishwa katika mkutano huo.

Habari hizo zinaeleza watakaotambulishwa siku hiyo ni wenyeviti wa CCM wa mikoa, wilaya na waliokuwa wabunge wa chama hicho ambao wanamuunga mkono Lowassa.

Jana Lowassa, aliyekuwa amevaa shati jeupe na suruali nyeusi na aliyekuwa katika gari aina ya Toyota Land Cruiser VX, alifika makao makuu ya Chadema saa 9:35 alasiri akiwa pamoja na familia yake na alipokewa na umati mkubwa wa watu waliokuwa wamebeba mabango yenye ujumbe mbalimbali.

Baadhi ya ujumbe huo ni “Chini ya Lowassa umaskini haupo”, “Kwa Lowassa hata maskini atapata ajira” na “Kingunge Ngombare-Mwiru karibu Ukawa”. Kingunge ni kada mkongwe wa CCM na anamuunga mkono Lowassa.

Mbali na kubeba mabango, watu hao walikuwa wakiimba nyimbo mbalimbali za kumsifu Lowassa na kushangilia pale ilipokuwa ikitajwa mikakati ya chama hicho kushika dola.

Kura milioni 1.6

Akieleza taratibu na kanuni za kudhamini mgombea urais, mkurugenzi wa Oganaizesheni na Mafunzo wa chama hicho, Benson Kigaira alisema mgombea urais anatakiwa kudhaminiwa na wanachama wasiopungua 200.

“Naamini fomu za Lowassa zitakuwa na idadi hiyo ya wadhamini. Ila baada ya mgombea kuchukua fomu jioni yake wanachama wa Chadema, wapenzi na Watanzania walifurika katika ofisi za Kanda, mikoa na majimbo nchi nzima wakiomba kumdhamini,” alisema Kigaira.

Alisema wanachama hao walidhani fomu hizo zimepelekwa kila mkoa, kutokana na kuepuka kuwanyima fursa hiyo chama hicho kilipeleka fomu ili wanachama wamdhamini na kupewa masharti kuwa lazima wawe wamejiandikisha kupiga kura, wataje namba zao za simu.

Huku akionyesha fomu chache za wadhamini kutoka mikoa mbalimbali nchini, Kigaira alitaja idadi ya watu waliomdhamini Lowassa katika mikoa yote 32 kuwa ni 1,662,397.
Akizungumzia udhamini wa wanachama Mwalimu alisema: “Lowassa alitakiwa azunguke mikoani kusaka wadhamini ila siku zilikuwa zimebaki mbili. Tuliwataka wanachama wanaotaka kumdhamini (Lowassa) wafike makao makuu, siku uliyochukua fomu. Wanachama 700 walikuja kukudhamini.”

Alisema kitendo hicho kiliiibua malalamiko kutoka kwa wanachama wa mikoa mbalimbali nchini, hivyo kuagizwa fomu za udhamini zipelekwe mikoani.

Safari ya Lowassa haitavurugwa

Katika maelezo yake, Mwalimu alisema CCM inafanya vikao ili kuivuruga Chadema, lakini akasema kuwa hilo halitafanikiwa na hakuna wa kuivuruga safari ya Lowassa.

“Tunajua kuna mikakati na vikao vinavyoendelea kwa nia ya kumzuia Lowassa katika safari hii ya Chadema na Ukawa, lakini tunawaambia Lowassa kuja Chadema ni mpango wa Mungu.
Hatujamuokota barabara, ni Mungu amemuongoza kuja chama chetu kwa sababu Mungu ameshakiandikia neema chama hiki kutokana na falsafa inazokisimamia tangu kuanzishwa kwake.”

“Njama zozote za kishetani, kihafidhina na kifedhuli zitalegea na kupotezwa. Lowassa amebakiza hatua mbili, ya kwanza ni kumaliza mchakato wa ndani ya chama kupitia Mkutano Mkuu na hatua ya pili ni kuapishwa.”

Mwalimu alisema Chadema inaunga mkono kauli ya Lowassa ya kuuchukia umaskini, kwamba nchi imeshindwa kupata maendeleo kutokana na kuongozwa na viongozi wa CCM wenye fikra za kimaskini, za kuamini ili uwe kiongozi lazima uwe maskini.

Alisema baada ya Lowassa kupitishwa na Mkutano Mkuu chama hicho, atazunguka mikoa mbalimbali nchini kuanzia Dar es Salaam Agosti 9.

Lengo ni kuchukua nchi

“Kuna watu walidhani Lowassa hawezi kurejesha fomu. Safari ya kuelekea uchaguzi mkuu imefikia hatua muhimu. Kinachofuata ni Kamati Kuu kupitisha fomu hizi. Naamini hakuna pingamizi lolote maana mpaka sasa hakuna aliyejitokeza kuchukua fomu za kugombea urais kupitia Chadema na Ukawa,” alisema Profesa Safari.

Alisema wapo wanaosema mwaka huu wapinzani wataambulia wabunge na madiwani tu siyo rais, jambo alilodai kuwa si kweli na kwamba lengo lao ni kushinda kiti cha urais.

“Wazanzibari wana msemo wao kwamba goli unafungwa, lakini chenga twawala. Sisi chenga
 tutapiga na magoli tutafunga,” alisema.

Vigogo CCM

Habari za ndani kutoka chama hicho zinaeleza kuwa vigogo wa CCM watatambulishwa kabla ya kuanza kwa Mkutano Mkuu wa chama hicho, wakiwemo wabunge mashuhuri.

“Siku ya mkutano mkuu watatambulisha wabunge na viongozi wa CCM. Ni wengi na wengine watawashangaza watu kwa kweli kwa sababu si watu wanaotarajiwa kuihama CCM, “ alisema mpashaji habari wetu.

Mbunge wa Arumeru Magharibi, Goodluck Ole Medeye ndiye anayeambatana na Lowassa na amehudhuria hafla zote za uchukuaji na urejeshaji fomu, mara zote akiulizwa amekuwa akijibu kuwa ni mshauri wa mbunge huyo wa Monduli wa masuala ya kupambana na rushwa.

Chizii agoma kuzungumza

Naye kada mkongwe wa CCM, Matson Chizii ambaye naye amekuwa bega kwa bega na Lowassa tangu ahamie Chadema, alipoulizwa kama amehamia katika chama hicho kikuu cha upinzani nchini alisema hana cha kujibu, kusisitiza kuwa atajibu suala hilo siku mbili zijazo.

Nape afafanua sakata lake na Takukuru Lindi


Nape Nnauye, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM
Lindi. Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye amefafanua sakata lake la kuchukuliwa na askari wa Takukuru kwa mahojiano muda mfupi baada ya kuchukua fedha benki, akisema alikuwa akielekea kulipa mawakala.

Nape, anayewania ubunge wa Jimbo la Mtama, jana mchana aliamriwa na maofisa wa Takukuru kufika ofisi zao baada ya kutoka kuchukua fedha benki ya NMB eneo la Misonobarini mkoa Lindi.
“Ninadhani hawa jamaa walipotoshwa. Mimi nimekwenda zangu benki kuchukua fedha, lengo langu ni kuwalipa mawakala,” alisema Nape jana jioni alipopigiwa simu na Mwananchi kutoa ufafanuzi wa sakata hilo.

“Wakaja hawa jamaa, wakajitambulisha kuwa wanatoka Takukuru, wakaniuliza ‘mbona ninachukua fedha nyingi kipindi hiki?’ Nikawaambia ‘nakwenda kulipa mawakala, na fedha zenyewe ni hizi Sh3.6 milioni’.
“Basi, tukatoka taratibu tukaenda ofisini kwao, ni karibu tu na benki. Wakanihoji hata haikumalizika nusu saa, niliwaambia nataka kulipa mawakala wangu, tena fedha zenyewe hazitoshi, wako zaidi ya 100.”

Nape aliongeza kusema kuwa walimkamata na akawaambia kuwa yeye ni mwadilifu.
“Halafu ninyi, mnaacha marushwa makubwa makubwa huko, watu wanahonga halafu mnamvizia Nape masikini kwa Sh3mil?,” alisema.
Nape alielezea kufadhaishwa na tukio hilo akidai kuwa limetengenezwa kwa ajili ya kumchafua hasa kwa kuwa leo kuna kura za maoni, lakini akasema anaamini yeye ni msafi.
Kamanda wa Takukuru wa Mkoa wa Lindi, Stephen Chami alikiri kumhoji Nape, lakini akasema walijiridhisha kuwa fedha hizo ni kwa ajili ya kulipa mawakala.

“Unajua tuna watu wetu, kwenye maeneo mbalimbali hasa kipindi hiki cha uchaguzi, tumeweka watu wetu maeneo mengi, tunataka kukomesha rushwa,” alisema.


Kilango ageuka ‘mbogo’
Katika hatua nyingine, Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Anne Kilango Malecela juzi aligeuka mbogo baada ya kuzushiwa katika mitandao ya kijamii kuwa anashikiliwa na polisi.
Taarifa hizo zilizosambazwa jana, zilidai kuwa Kilango alikamatwa juzi saa 5:00 usiku katika eneo la Dimbi, kijiji cha Bagamoyo kwa tuhuma za kutoa rushwa, madai ambayo ameyakanusha.
Hata hivyo, Kilango alipoulizwa jana alisema tuhuma hizo ni uzushi uliotengenezwa na baadhi ya washindani wake wakiamini kwa kufanya hivyo watamvurugia katika kura ya maoni inayofanyika leo.

“Sijakamatwa na wala sijaona hata polisi mmoja nyumbani kwangu. Nimelala nyumbani kwangu jana (juzi) na leo (jana) nimeamka nyumbani kwangu na niko kwenye mikutano ya kuomba kura,” alisema.
Kilango aliongeza,”Sasa hivi nimetoka kuomba kura Mtii nilikuwa peke yangu wagombea wanzangu wameingia mitini. Niko Bombo sasa hivi (saa 9;00 alasiri) ndio wanakuja nishapiga bao.”
Kwa mujibu wa Kilango, baadhi ya wagombea wamekuwa wakifanya kampeni zisizo za kistaarabu kwa kuandaa vijana aliodai wamepewa pombe ili wamzomee katika baadhi ya maeneo aliyopita.

Wakati headlines za Dr. Slaa zikiendelea na CHADEMA, haya ni maneno 28 kayaandika Zitto Kabwe

ZZK 

Kumekuwa na Headlines nyingi mfululizo kuhusu kinachoendelea CHADEMA baada ya kupokelewa kwa Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli, Edward Ngoyai Lowassa… swali ambalo ripota wa kelvinmatemba.com alimuuliza Mbunge Tundu Lissu kuhusu ishu ya mpasuko ambayo iliandikwa sana Magazetini, jibu lake lilikuwa hili  >>>> “Haya maneno ni ya siku nyingi sana na tumetabiriwa maafa tangu siku ya kwanza… Lowassa hakukaribishwa na Mwenyekiti wa CHADEMA pekeyake, Wenyeviti wa UKAWA wote walikuwepo kwenye stage. Anaesema UKAWA imeteteleka hayo maneno hayataisha” — Tundu Lissu.
Magazeti yameendelea kuandika kuhusu stori ya kinachoendelea CHADEMA, gazeti la Raia Tanzania August 01 2015 limebeba headline hii >>> “Dk. Slaa ajivua uanachama, ni siku chache baada ya kujiuzulu Ukatibu Mkuu, arejesha nyaraka, gari” >>>
ZITTO
Zitto Kabwe amepost picha ya gazeti hilo @Instagram na kuyaandika haya >>> Siasa zinabadilika sana. Siamini kama hili laweza kutokea, lakini wiki kwenye siasa ni kubwa mno. Sisi wengine tunatazama tu maana tulipita kwenye changamoto hizi“– @
Zitto Kabwe

Rais Mugabe atimua walinzi wake 27 baada ya kuanguka


Rais Robert Mugabe akiwa chini baada ya
Rais Robert Mugabe akiwa chini baada ya kuanguka hivi karibuni. Picha maktaba 


Harare, Zimbabwe. Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe amewasimamisha kazi walinzi wake 27 ikiwa ni siku chache baada ya kuanguka katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Harare wakati akirejea nyumbani akitokea Addis Ababa, Ethiopia.
Kati ya waliokumbwa na adhabu hiyo ni pamoja na walinzi wake wa karibu ambao wanadaiwa kutojishughulisha kwa lolote wakati kiongozi huyo alipoteleza na baadaye kuanguka chini.
Likiwanukuu maofisa wa serikali, gazeti la The Standard lilisema kuwa walinzi hao wamewajibishwa kwa kushindwa kuchukua hatua za dharura kushughulikia tukio hilo lililosambaa katika mitandao ya kijamii.
Rais Mugabe ambaye alikutwa na mkasa huo muda mfupi baada ya kuzungumza na wafuasi wake waliokuja kumpongeza baada ya kuchaguliwa kuwa mwenyekiti wa Umoja wa Afrika wiki ijayo atasherehekea siku yake ya kuzaliwa akitimiza miaka 91.
Vyanzo vya habari vinasema kuwa, Ikulu haikufurahishwa na namna walinzi wake walivyoshindwa kuchukua hatua za haraka kudhibiti kuenea kwa taarifa za kuanguka kwake.
Taarifa zimesema kuwa kwa ujumla walinzi wa rais walibweteka kwani kanuni zinawataka kusimama angalau hatua chache kutoka kiongozi alipo.
“Hili suala ni kubwa  tena lilipaswa kushughulikiwa kwa umakini mkubwa na hawa walinzi walizembea kwani kanuni namba tatu inayohusu ulinzi kwa rais inaeleza ni umbali gani wanapaswa kusimama.  Ninachoweza kusema ni kwamba  kuna idara nyingi zinaendelea kuchunguzwa, kuanzia Shirika la Ndege la Zimbabwe lenyewe  hadi timu nzima ya walinzi wake.
 Sina uhakika katika hawa waliosimamishwa kama kuna mmoja wao atarejea kazini,” kilisema chanzo kimoja cha habari kikikariri taarifa kutoka  mtandao wa www.bulawayo24.com.  Hata hivyo mtandao huo baadaye ulisema kuwa taarifa ofisi ya Ikulu imekanusha vikali taarifa hizo.
Taarifa zaidi zinasema kuwa walinzi hao walikabidhiwa barua za kusimamishwa kazi mwishoni mwa wiki na kwamba kurejea kwao kutategemea uchunguzi unaoendelea kufanywa.
Taarifa za kuwa walinzi hao walikuwa wamesimamishwa kazi zilipata nguvu mpya wakati wa ziara ya Rais Edgar Lungu wa Zambia aliyekuwa nchini Zimbabwe na kukutana na mwenyeji wake Rais Mugabe.
Wale waliokuwepo Ikulu walisema kuwa walishuhudia sura mpya za walinzi wakiwa kando ya Rais Mugabe. Hata wakati Rais Lungu akiondoka Ikulu, Rais Mugabe hakuambatana naye kumsindikiza uwanja wa ndege badala yake alisimama mita chache na baada ya mgeni wake kuondoka alirejea tena ofisini.
Msemaji wa Ikulu George Charamba hata hivyo alipuuza taarifa hizo akisema kuwa ni uzushi unaoenezwa na watu wasiokuwa na tija.
Alisisitiza kuwa hakuna mlinzi yoyote wa rais wala ofisa wa Ikulu aliyesimamishwa kazi kutokana na tukio la kuanguka kwa Rais.
Rais Mugabe ambaye anatajwa kuwa ni miongoni mwa viongozi wachache barani Afrika waliokaa madarakani kwa muda mrefu wiki iliyopita alichaguliwa kuwa mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU) wadhifa ambao ulizua hali ya wasiwasi kuhusu nafasi ya umoja huo katika jumuiya ya kimataifa.
Hata hivyo hivi karibuni Umoja wa Ulaya ulisema kuwa utalegeza vikwazo kwa kiongozi huyo ili aweze kuhudhuria baadhi ya mikutano ya kikanda hasa ile inayohusu Umoja wa Afrika na jumuiya ya kimataifa.